• Malalamiko |
    • MAWASILIANO |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Wafanyakazi |
Kaliua District Council
Kaliua District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu, na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
      • Usafi wa Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Legal Unity
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji

HALMASHAURI NCHINI ZASHAURIWA KUIGA MFANO KALIUA

Posted on: April 25th, 2018

Kiongozi wa mbio za mwenge 2018 Ndugu Charles Francis Kabeho, amezishauri Halmashauri nchini kuiga mfano kwa Halmashauri ya Kaliua. Akihitimisha zoezi la uwekaji mawe ya msingi na uzinduzi wa miradi Kabeho amesema kuwa ameridhishwa na usimamizi wa miradi na matumizi fedha za miradi yote aliyoitembelea kwani inaakisi thamani ya fedha (value for money) iliyotolewa na serikali pamoja na wahisani.

“Nampongeza sana Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji na wote walioshiriki katika usimamizi wa miradi hapa Kaliua” Alisema.

Mwenge wa uhuru ulipokelewa tarehe 24 Aprili katika eneo la Isawima ukitokea mkoani kigoma na kukimbizwa na wananchi katika vijiji vya Kaliua Magharibi, Imalampaka na Kaliua Mashariki.

Mbio za mwenge zimeweka mawe ya msingi na kuzindua jumla ya miradi nane yenye thamani ya shilingi 1,870,467,033.33 kutoka serikali kuu, Halmashauri, michango ya wananchi na wahisani.

Miradi iliyozinduliwa ni Jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua na Kiwanda cha mashine za kubangua karanga cha mtu binafsi Ndugu Fanuel Shao.

Wakati miradi iliyowekewa mawe ya msingi ni; Jengo la Upasuaji katika Kituo cha Afya Kaliua, Bweni la kulala wavulana shule ya sekondari Kaliua na Upanuzi wa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia nafaka kwa Ndugu Jumanne Lusaba.

Miradi mingine iliyowekewa mawe ya msingi ni ujenzi wa stendi ya mabasi, egesho la malori na kibanda cha abiria pamoja na Mradi wa ujenzi wa barabara kilometa moja kwa kiwango cha lami. Vile vile mwenge wa uhuru ulikagua mabanda ya upimaji wa UKIMWI/VVU, Banda la wapinga rushwa, wapinga matumizi madawa ya kulevya, banda la wajasiriamali vijana na wanawake na kutoa zawadi za washindi wa mpira wa miguu wa ligi ya mwenge. Sambamba na uzinduzi wa miradi wakimbiza mwenge walipata fursa ya kupanda miti katika maeneo mbalimbali.

Wananchi wa Kaliua walishiriki katika mkesha wa sherehe za mwenge uliofanyika katika viwanja vya Kolimba na kuwapa fursa ya kupima virusi vya ukimwi malaria na kuchangia damu.

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Mh. Abel Yeji Busalama amehitimisha mbio za mwenge wilayani kaliua na kuukabidhi mwenge kwa Mkuu wa wilaya ya Urambo Bi. Angelina Kwingwa 25.04.2018 ukiwa unawaka na kumeremeta.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI KALIUA DC MSAIDIZI WA HESABU DARAJA LA II November 17, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KALIUA May 25, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KALIUA May 25, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KALIUA May 25, 2022
  • Ona zote

Habari za Hivipunde

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA DEREVA WA MTAMBO DARAJA LA II {GREDA} NAFASI 01

    May 04, 2025
  • MNADA WA KWANZA WA ZAO LA KARANGA WILAYA YA KALIUA

    March 24, 2025
  • MADIWANI KALIUA WAPITISHA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA BAJETI YA BILION 50.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    January 30, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KALIUA KUPITIA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII IMETOA HUNDI YA TSH. 302,000,000/=

    December 23, 2024
  • Ona zote

Video

Karibu Mwenge wa Uhuru Wilayani Kaliua 2018
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mwanzo
  • TAMISEMI
  • Huduma
  • Historia
  • Fursa za Uwekezaji
  • UTUMISHI

Kurasa zinazofanana

  • Salary Slips Portal
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya RC Tabora
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti za Serikali
  • Baraza la Mitihani - NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

MAWASILIANO

    Ofisi zipo Eneo la Ufukutwa, Barabara ya Ulindwanoni

    Sanduku La Posta: S. L. P 83 Kaliua

    Simu: +255262965676/9

    Dawati la Uwekezaji:

    Barua Pepe: ded@kaliuadc.go.tz

Dawati la Malamiko

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Service

Hatimiliki ©2016 Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua